Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Musalia Mudavadi amefichua kwamba Wakenya 16 wamepotea nchini Urusi baada ya kujiunga na jeshi la nchi hiyo, huku wengine 47 wamerudi nyumbani kutoka vitani nchini Ukraine.

Akizungumza katika mkutano wa kamati ya seneti, Mudavadi alisema kwamba Wakenya wengine 38 wako katika hospitali mbalimbali nchini Urusi chini ya ulinzi mkali. Idadi ya watu waliofariki dunia imeongezeka kutoka 10 hadi 16 katika masaa 24 yaliyopita, na bado haijuliki kama wako hai au wamefariki.
Waziri alikadiria kuwa Wakenya 165 wanashiriki katika operesheni za kijeshi, hivyo kuifanya idadi ya Wakenya wanaoshiriki katika mgogoro wa Ukraine ziwe zaidi ya 250. Mudavadi aliongeza kuwa idadi halisi inaweza kuwa kubwa zaidi. Alithibitisha pia kuwa Wakenya wawili wanashikiliwa kama wafungwa wa vita na Ukraine.
Wale walioajiriwa walisaini mikataba ya kufanya kazi kama maofisa wa usafirishaji au majukumu ya mapigano. Kwa mujibu wa waziri, wakala wa ajira walioko Kenya, Urusi, Qatar, na Falme za Kiarabu wana husika na mpango huu wa uajiri. Kenya imefungua uchunguzi kuhusu uajiri haramu wa raia wake kupigana katika vita vya Ukraine.
Chanzo: BBC Africa
Picha: BBC Africa


